Friday 7 June 2013

HIVI NDIVYO BIKRA FEKI ZINAVYOTENGENEZWA

BIKRA FEKI

WANAUME,kuweni makini na Bikra feki...Wanawake wana mbinu nyingi sana za kukuingiza kingi,ndoa imekuwa mtihani kwao,wanafanya kila balaa ili wakuchote akili uingie kingi.Ukiacha hawa wengne ambao wameamua kuwa Washirikina kwa kwenda kwa Waganga na kupewa dawa za kukukamata,kuna hawa wanawake ambao wametumika kama Bajaj za Salasala,wakikuona umekaa dizaini ya muoaji halafu una hela,utapigwa tukio mpaka ushangae.Atajifanya descent na hajui kitu,atasingizia yeye bikira au amefanya mara moja tu...OGOPA SANA!
Siku ya kufanya Mapenzi kila ukimshika anapiga kelele za kuzuga anaumia,ukishika nywele analia...ukimgusa kifua anapiga yowe kama anakeketwa,ukianza kuzama ndo kabisa,unaweza kudhani uko kwenye Msiba wa Kinyakyusa....utasikia taratibu,utafinywa,utapushiwa kama vile ndo unaitoa,kumbe wala...
Mtu mzima unachotwa akili kumbe mwenzio kabla hajaja amekamulia Ndimu,mchanganyiko wa parachichi na tikiti maji,Sabuni ya Kaisiki na Vim ya kuondolea harufu chooni...Ukigusa unahisi bikira kumbe wala,umetegwa...Hawaruhusu uingize kidole kwenye maandalizi hata kwa dawa utagundua...dawa yao unakaa na beseni,akizuga unamwagia maji pale juu,litatoka vumbi hujawahi kuona hata kwenye stoo yenu ya kuku wa mayai...BEWARE na hizi bikira za makuti!

Saturday 1 June 2013

HOW TO GET A GIRLS NUMBER

HOW TO TALK TO A GIRL YOU DONT KNOW

Fanya haya! Unapotokea kumpenda mtu aliye na mpenzi wake,.

Tumshukuru Mwenyezi Mungu ambaye ametuwezesha kuonana tena wiki hii tukiwa wazima. Lakini pia tumshukuru kwa kutuletea kitu kinachoitwa mapenzi.

Mapenzi yamekuwa yakichukua nafasi kubwa sana katika maisha yetu ya kila siku na yamekuwa yakichangia kwa kiasi kikubwa furaha kwa kila mtu.


Kama huamini, angalia wale waliotokea kupenda na wao wakapendwa, utabaini nyuso zao zimetawaliwa na

furaha isiyo na kifani. Lakini mapenzi hayo hayo yamekuwa ni chanzo cha vilio kwa baadhi ya watu.

Mpenzi msomaji wangu, kupenda hakuna macho! Moyo ukishapenda hausikii la kuambiwa. Katika hili ndiyo maana unaweza kumuona mwanaume kazimika kwa demu ambaye hawaendani kabisa lakini moyo wake ndiyo umeshapenda.


Ilishawahi kutokea msichana akampenda kijana mmoja ambaye ni fukara kupita maelezo. Yeye akawa ndiyo anamhudumia kwa kila kitu. Akamfanyia mpango wa ajira na mwisho wake wakafunga ndoa.


Sasa hivi wanaishi maisha ya furaha na amani. Wamegeuka mfano wa kuigwa kwa jinsi wanavyopendana lakini huko nyuma msichana huyo alikuwa akichekwa kwa kutoa penzi kwa mwanaume asiye na mbele wala nyuma.


Hayo ndiyo mapenzi jamani! Lakini pia katika kufurukuta kumtafuta mpenzi wa kuwa naye maishani, mwanaume anaweza kujikuta unaangukia kwa demu ambaye tayari ana mpenzi wake.


Moyo wako unakuambia yeye ndiye mtu sahihi katika maisha yako lakini tayari ana mtu wake, unafanyaje?


Utapambana kuhakikisha unapata kile ambacho moyo wako umekipenda au utakubaliana na ukweli kwamba huwezi kuwa naye kwa kuwa ana mtu wake? Inapofikia hatua hiyo unaweza kujikuta upo njia panda hasa pale ambapo huyo mwenye mtu wake naye anaonesha kuwa na chembechembe za mapenzi kwako.

Kuna mambo kadhaa ya kukusaidia kukabiliana na hali hii.


Chunguza

Tumia muda wako mwingi kuchunguza juu ya uhusiano wake. Uhusiano wao umesimama na wanaonekana ni watu wenye ‘future’? Nasema hivyo kwa sababu, yawezekana uhusiano wa huyo uliyetokea kumpenda ni wa kuzuga tu na huenda wewe ndiye mwenye ‘future’ naye. Ndiyo maana nikasema chunguza uhusiano wake kwanza.


Usitafute uadui

Baada ya kuchunguza, ukibaini kwamba uhusiano wao hauko ‘siriasi’, vuta subira, lolote linaweza kutokea na likaufurahisha moyo wako. Lakini kama utaona ni watu walio siriasi na wanaelekea kuoana, usitafute uadui bure, kaa pembeni.


Una nafasi kwake?

Sawa umetokea kumpenda msichana aliye na mtu wake, umeshawahi kujiuliza kama una nafasi ndani ya moyo wake? Anaonesha dalili fulani za kukupenda kama unavyompenda na ni mtu anayeonesha kukumisi anapokuwa mbali na wewe? Utakapobaini una nafasi kwake, uamuzi wa kumpotezea hautakuwa na nafasi.


Ni rahisi kubadili uamuzi wake?

Unadhani huyo uliyetokea kumpenda anaweza kubadili maamuzi ya kumuacha huyo aliyenaye kama kweli hawana ‘future’? Utagundua hilo kwa kuongea naye na kumsikia kama anaweza kufanya maamuzi hayo ili awe na wewe.


Pingana na moyo wako

Ifike wakati upingane na moyo wako. Unajua moyo wako kukuambia kuwa unataka kuwa na uhusiano na demu ambaye tayari ana mpenzi wake wakati mwingine utakuwa unakupotosha.


Kwa hiyo ukiona vipi, pingana nao. Acha kumng’ang’ania msichana mwenye mpenzi wake licha ya ukweli kwamba, huenda wewe ndiye mwenye nafasi ya kuwa mume wake na siyo huyo aliye naye.


Urafiki ni poa?

Umempenda sana na hauko tayari kumkosa katika maisha yako lakini imetokea kwamba tayari yuko na mtu na umebaini huna nafasi kwake kabisa? Usiumie, omba angalau urafiki. Siyo urafiki wa kivile sana ila angalau pale unapotaka kusikia sauti yake kwa kumsalimia tu, upate nafasi hiyo.


Usiumie, yupo mwingine

Haina haja ya kujitafutia vidonda vya tumbo bure kwa kuwa tu umebaini uliyetokea kumpenda tayari ana mtu. Chukulia ni hali ya kawaida, mademu wazuri ambao wanaishi singo wapo kibao huko mtaani, ni suala la wewe kutulia tu. Amini yupo mwingine ambaye atayafanya maisha yako yawe ya furaha.


Naomba nihitimishe kwa kusema kwamba, unapotokea kumpenda mtu fulani, pambana kuhakikisha unampata kwa sababu ukimkosa maisha yako yanaweza kuwa gizani. Ila pale utakapoona uwezekano wa kuwa naye haupo, usilazimishe ndugu yangu. Kumbuka haya ni maisha tu!

SASA UNAWEZA KUISIKILIZA CLOUDS FM LIVE ON AIR KUPITIA simonbango.blogspot.com & irypine.blogspot.com KOKOTE DUNIANI