Wednesday 2 October 2013

JINSI YA KUJIZUIA USIPATE SARATANI YA MATITI (BREAST CANCER) KWA KUFANYA HAYA


1. JICHUNGUZE MATITI YAKO.
Ukijichunguza mwenyewe mapema inasaidia
kugundua saratani mapema na kutibika kwa
urahisi, unatakiwa kujichunguza walau mara
moja kwa mwezi baada ya wiki moja ya
kwanza kupita baada ya hedhi, na wasiopata
hedhi wajichunguze tarehe za mwanzo wa
mwezi, unapo kandamiza ziwa lako kwa
ndani ukihisi kuna uvimbe au nundu(kitu
kingumu) na maumivu,basi fanya mapema
ukamwone daktari kwa uchunguzi zaidi.


2. Mammogram (Hiki ni kifaa chenye uwezo wa
kuonesha uvimbe ndani ya titi)
Wanawake wenye umri zaidi ya miaka 40
wanashauriwa kufanya hiki kipimo walau
mara moja kwa mwaka hata kama kwenye
familia yake hakuja wahi kuwa na tatizo la
saratani ya matiti, wanawake wanashauriwa
kuanza kipimo hiki katika umri wa miaka 30
kama kwenye familia yake dada au mama
yake alikuwa na saratani ya matiti.

3.MAMA KAMA ANA MTOTO ANAYE NYONYA
USIACHE KUMNYONYESHA
Wanawake wengi katika ulimwengu wa
kisasa huacha kunyonyesha watoto maziwa
wakiofia kualibu muonekano wa maumbile
yao, hii ni hatari kwani huongeza hatari ya
kupata saratani ya matiti, uchunguzi
unaonesha kwamba akina mama
wanaonyonyesha watoto wao mpaka umri wa
miaka 2 huzuia hatari ya kupata saratani ya
matiti kwa 60%, sababu ni kwamba
kunyonyesha mtoto hupunguza mizunguko
ya siku za hedhi na hupunguza kiasi cha
estrogen ambayo husababisha kansa.

4. KUWA NA UZITO WA KAWAIDA
Wanawake ambao wana maumbo makubwa
yani unene wanapofikia (menopause) ni
kipindi ambacho hawezi kuzaa tena huwa
katika hatari ya kupata saratani ya matiti,
kabla ya kufikia kipindi hichi mirija ya uzazi
ndiyo hutengeneza estrogen na kiasi kidogo
tu hutengenezwa na seli za mwili. Baada ya
menopause, mirija ya uzazi huacha
kutengeneza estrogen hapo sasa estrogen
hutengenezwa na mafuta ya mwili, kuwa na
mafuta mwilini mengi maana yake pia una
estrogen nyingi ambao hupelekea saratani ya
matiti. Kwa afya nzuri mwanamke
anashauriwa kuwa na BMI chini ya 25.

5. KUPIMO CHA MAGONJWA YA KURITHI(GENETIC
TESTS)
Ni pekee 5 hadi 10% ya saratani ya matiti
husababishwa kutoka mabadiliko ya ghafla ya
jene kutokana na kurithishwa jene za kansa
(gene mutations).

6. KUFANYA MAZOEZI
Kufanya mazoezi pia kuna punguza hatari ya
kupata saratani ya matiti fanya mazoezi walau
dakika 30 kwa wiki mara tatu, hii itasaidia
kuunguza mafuta mwilini, kuwa mwepesi na
kuongeza kinga ya mwili. Mazoezi
yanashusha kiwango cha estrogen , na
mazoezi yanapunguza hatari ya saratani ya
matiti kwa 20 hadi 40%, pia unaweza
kufanya mazoezi ya kuongeza pumzi kwa
kutembea haraka.

7. KULA VYAKULA VISIVYO KUWA NA MAFUTA MENGI.
Vyakula visivyo kuwa na mafuta mengi
hupunguza hatari ya saratani ya matiti,
humfanya mtu asi nenepa. Kwani kiasi cha
mafuta mwilini kikiwa kingi huleta saratani ya
matiti.

8. PUNGUZA KIASI CHA POMBE UNACHOKUNYWA
(KI LEVI)
Punguza kiasi cha pombe unachotumia kwani
sumu iliyopo kwenye kilevi huenda moja kwa
moja kushambulia DNA ambapo husababisha
kansa, mwanamke anaye kunywa bia 2 hadi
5 kila siku huzidisha 1.5 ya hatari kupata
saratani ya matiti, ukilinganisha na asiye
kunywa pombe, acha kabisa unywaji wa
pombe ikiwezekana tumia bia 1 tu kwa siku
kwa ajili ya afya.

9. KULA MAHARAGE YA SOYA
Kula maharage soya na viginge vinavyofanana
na soya itapunguza hatari ya saratani ya
maziwa, soya ina mchanganyiko wa
isoflavones hii huungana na seli za mwili na
kuizuia estrogen kutengeneza seli za saratani
ya matiti.

10. USIWE KARIBU NA DAWA ZA KUUA WADUU NA
KEMIKALI ZA AINA YEYOTE.
Usiwe navyo karibu kwani zina tabia kama
estrogen ambazo husababisha seli za saratani
za matiti kujizalisha haraka, pia husababisha
ugonjwa kuenea haraka.

11. PUNGUZA KIASI CHA MIONZI
Wanawake waliofanyiwa matibabu ya mionzi
kwenye kifua kama ugonjwa wa Hodgkin`s
na non-hodgkin`s lymphoma au acne wapo
katika hatari ya kupata saratani ya matiti, kiasi
cha kupata saratani ya matiti kwa mionzi
inategemea na umri, walio na umri ya miaka
zaidi ya 40 wakipata matibabu yoyote yale ya
mionzi hawaongezi hatari ya kupata na
saratani ya matiti.
source-manyandahealthy

MAZOEZI 3 YA KUZUIA MATITI YA MWANAMKE YASILALE NA KUWA MALAPA....SOMA HATA KAMA YAMELALA...

Ikiwa wewe umechelewa(ulikuwa hujui hili wakati matiti yako yanaota) basi msaidie mdogo wako au binti yako anaekuwa hivi sasa, ili asije kujisikia vibaya pale wanaume watakapokuwa wakiponda  matiti kwa kuyaita "malapa"....



Kwanza kabisa hakikisha mtindo wa kulala ni kifudifudi (kulalia tumbo), kwa kufanya hivyo kunasaidia kwa kiasi kikuwa kufanya matiti yako pumzike, kwamba hakutakuwa na kuning'inia kama utakuwa umelala chali(lalia mgongo) au kiubavu.

Zoezi...1
Asimame wima dhidi ya mlango au ukuta kisha aegeshe matiti yake mahali hapo kwa nguvu kisha aachie (ajitoe ukutani), zoezi hili hufanya matiti yaume sana lakini wewe kama dada  mpe moyo kuwa avumilie. Afanye hivyo mara 20 kila asubuhi.

Zoezi....2
Simama wima huku mikono yako ikiwa imenyooshwa huku na kule kisha ipeleke mbele nakukutanisha viganja vyako alafu irudishe nyumba kadiri uwezavyo (sio lazima ikutane) ila utahisi maumivu fulani sehemu ya matiti (misuli yafanya kazi hapo)....fanya hivyo mara 10 na ongeza hesabu njinsi unavyokua.

Zoezi...3
Ukiwa umesimama wima na mikono yako imenyooshwa huku na hule inanyue taratibu kuelekea juu na kutanisha vidole vyako huko juu kisha rudisha mikono ilipokuwa (imenyooka huku na kule).

Friday 7 June 2013

HIVI NDIVYO BIKRA FEKI ZINAVYOTENGENEZWA

BIKRA FEKI

WANAUME,kuweni makini na Bikra feki...Wanawake wana mbinu nyingi sana za kukuingiza kingi,ndoa imekuwa mtihani kwao,wanafanya kila balaa ili wakuchote akili uingie kingi.Ukiacha hawa wengne ambao wameamua kuwa Washirikina kwa kwenda kwa Waganga na kupewa dawa za kukukamata,kuna hawa wanawake ambao wametumika kama Bajaj za Salasala,wakikuona umekaa dizaini ya muoaji halafu una hela,utapigwa tukio mpaka ushangae.Atajifanya descent na hajui kitu,atasingizia yeye bikira au amefanya mara moja tu...OGOPA SANA!
Siku ya kufanya Mapenzi kila ukimshika anapiga kelele za kuzuga anaumia,ukishika nywele analia...ukimgusa kifua anapiga yowe kama anakeketwa,ukianza kuzama ndo kabisa,unaweza kudhani uko kwenye Msiba wa Kinyakyusa....utasikia taratibu,utafinywa,utapushiwa kama vile ndo unaitoa,kumbe wala...
Mtu mzima unachotwa akili kumbe mwenzio kabla hajaja amekamulia Ndimu,mchanganyiko wa parachichi na tikiti maji,Sabuni ya Kaisiki na Vim ya kuondolea harufu chooni...Ukigusa unahisi bikira kumbe wala,umetegwa...Hawaruhusu uingize kidole kwenye maandalizi hata kwa dawa utagundua...dawa yao unakaa na beseni,akizuga unamwagia maji pale juu,litatoka vumbi hujawahi kuona hata kwenye stoo yenu ya kuku wa mayai...BEWARE na hizi bikira za makuti!

Saturday 1 June 2013

HOW TO GET A GIRLS NUMBER

HOW TO TALK TO A GIRL YOU DONT KNOW

Fanya haya! Unapotokea kumpenda mtu aliye na mpenzi wake,.

Tumshukuru Mwenyezi Mungu ambaye ametuwezesha kuonana tena wiki hii tukiwa wazima. Lakini pia tumshukuru kwa kutuletea kitu kinachoitwa mapenzi.

Mapenzi yamekuwa yakichukua nafasi kubwa sana katika maisha yetu ya kila siku na yamekuwa yakichangia kwa kiasi kikubwa furaha kwa kila mtu.


Kama huamini, angalia wale waliotokea kupenda na wao wakapendwa, utabaini nyuso zao zimetawaliwa na

furaha isiyo na kifani. Lakini mapenzi hayo hayo yamekuwa ni chanzo cha vilio kwa baadhi ya watu.

Mpenzi msomaji wangu, kupenda hakuna macho! Moyo ukishapenda hausikii la kuambiwa. Katika hili ndiyo maana unaweza kumuona mwanaume kazimika kwa demu ambaye hawaendani kabisa lakini moyo wake ndiyo umeshapenda.


Ilishawahi kutokea msichana akampenda kijana mmoja ambaye ni fukara kupita maelezo. Yeye akawa ndiyo anamhudumia kwa kila kitu. Akamfanyia mpango wa ajira na mwisho wake wakafunga ndoa.


Sasa hivi wanaishi maisha ya furaha na amani. Wamegeuka mfano wa kuigwa kwa jinsi wanavyopendana lakini huko nyuma msichana huyo alikuwa akichekwa kwa kutoa penzi kwa mwanaume asiye na mbele wala nyuma.


Hayo ndiyo mapenzi jamani! Lakini pia katika kufurukuta kumtafuta mpenzi wa kuwa naye maishani, mwanaume anaweza kujikuta unaangukia kwa demu ambaye tayari ana mpenzi wake.


Moyo wako unakuambia yeye ndiye mtu sahihi katika maisha yako lakini tayari ana mtu wake, unafanyaje?


Utapambana kuhakikisha unapata kile ambacho moyo wako umekipenda au utakubaliana na ukweli kwamba huwezi kuwa naye kwa kuwa ana mtu wake? Inapofikia hatua hiyo unaweza kujikuta upo njia panda hasa pale ambapo huyo mwenye mtu wake naye anaonesha kuwa na chembechembe za mapenzi kwako.

Kuna mambo kadhaa ya kukusaidia kukabiliana na hali hii.


Chunguza

Tumia muda wako mwingi kuchunguza juu ya uhusiano wake. Uhusiano wao umesimama na wanaonekana ni watu wenye ‘future’? Nasema hivyo kwa sababu, yawezekana uhusiano wa huyo uliyetokea kumpenda ni wa kuzuga tu na huenda wewe ndiye mwenye ‘future’ naye. Ndiyo maana nikasema chunguza uhusiano wake kwanza.


Usitafute uadui

Baada ya kuchunguza, ukibaini kwamba uhusiano wao hauko ‘siriasi’, vuta subira, lolote linaweza kutokea na likaufurahisha moyo wako. Lakini kama utaona ni watu walio siriasi na wanaelekea kuoana, usitafute uadui bure, kaa pembeni.


Una nafasi kwake?

Sawa umetokea kumpenda msichana aliye na mtu wake, umeshawahi kujiuliza kama una nafasi ndani ya moyo wake? Anaonesha dalili fulani za kukupenda kama unavyompenda na ni mtu anayeonesha kukumisi anapokuwa mbali na wewe? Utakapobaini una nafasi kwake, uamuzi wa kumpotezea hautakuwa na nafasi.


Ni rahisi kubadili uamuzi wake?

Unadhani huyo uliyetokea kumpenda anaweza kubadili maamuzi ya kumuacha huyo aliyenaye kama kweli hawana ‘future’? Utagundua hilo kwa kuongea naye na kumsikia kama anaweza kufanya maamuzi hayo ili awe na wewe.


Pingana na moyo wako

Ifike wakati upingane na moyo wako. Unajua moyo wako kukuambia kuwa unataka kuwa na uhusiano na demu ambaye tayari ana mpenzi wake wakati mwingine utakuwa unakupotosha.


Kwa hiyo ukiona vipi, pingana nao. Acha kumng’ang’ania msichana mwenye mpenzi wake licha ya ukweli kwamba, huenda wewe ndiye mwenye nafasi ya kuwa mume wake na siyo huyo aliye naye.


Urafiki ni poa?

Umempenda sana na hauko tayari kumkosa katika maisha yako lakini imetokea kwamba tayari yuko na mtu na umebaini huna nafasi kwake kabisa? Usiumie, omba angalau urafiki. Siyo urafiki wa kivile sana ila angalau pale unapotaka kusikia sauti yake kwa kumsalimia tu, upate nafasi hiyo.


Usiumie, yupo mwingine

Haina haja ya kujitafutia vidonda vya tumbo bure kwa kuwa tu umebaini uliyetokea kumpenda tayari ana mtu. Chukulia ni hali ya kawaida, mademu wazuri ambao wanaishi singo wapo kibao huko mtaani, ni suala la wewe kutulia tu. Amini yupo mwingine ambaye atayafanya maisha yako yawe ya furaha.


Naomba nihitimishe kwa kusema kwamba, unapotokea kumpenda mtu fulani, pambana kuhakikisha unampata kwa sababu ukimkosa maisha yako yanaweza kuwa gizani. Ila pale utakapoona uwezekano wa kuwa naye haupo, usilazimishe ndugu yangu. Kumbuka haya ni maisha tu!

SASA UNAWEZA KUISIKILIZA CLOUDS FM LIVE ON AIR KUPITIA simonbango.blogspot.com & irypine.blogspot.com KOKOTE DUNIANI

Wednesday 29 May 2013

NAY WA MITEGO & DIAMOND WALIVYOWEKA HISTORIA NDANI YA MAISHA CLUB.......



Zifuatazo Ni Picha Zote za Matukio ya Jana kwenye
Video Launching ya Muziki Gani..
....
My super dancer Kushoto Moses Iyobo Kati Rama mpauka
 & Emma Platnum wakiwa
na Vijana wanaotengeneza Nguo za
Kundi zima la WASAFII wakati wowote wa show yoyote.......
Hatuelewi mpaka now watoboa Pua awajawasili.......
''Kijana umejipanga leo,usitegeme viuno vitakusaidia
 leo stejini'' Nay akimsalimu Diamond alipowasili
Maisha Club.....
Tukiwasili Maisha Club nikiwa na Crew yangu nzima
 ya wasafi na Nay wa Mitego
pembeni with Mkong'oto Jazz Band.....
Hapa ndipo kwenye Uhusika zaidi....Black & White
Carpets......Diamond Platnum
 & Nay wa Mitego....

Abdallah....On set Planet Bongo........

Hahahahahhaa Dimpoz bhana.......ACHA tu huyu jamaa 
asingekuwa Mwanamuziki angekuwa 
Comedian.......

True Boy akizungumza nao fans wake.......
wa Manzese Hammi.....


Aaanhaaa...... Maisha Mtanielewa asa hivi au Baadae....'' 
Nay akiwauliza mashabiki waliofurika
Ukumbini humo.....
Hyperman H.K ndo alikuwa msema chochote on the stage
 kusukuma Gurudumu...
Wasafi wakaanza kufanya Balaa lao taratibu......


Tuimbe wote sasa.....Maisha Lets Go......










Tuendeleeee ama tusiendeleeeeee............?




Kizai zai......ni mwendo wa viuno tu stejini......



\
Si ndio Diamond na Nay wakaanza kufanya yao stejini.....



Palikuwa Hapatoshi hapa kati....Patashika nguo kuchanika.....
Si ndio nikajua tayari Mwana Hip Hop Nshambadilisha.....ni mwendo
wa kudono donoa tu.....
QBoy Msafiii along side with Ommy Dimpoz kwa pozi,B
ckstage muda mchache baada ya
Show.....
Baada ya show.....Interview kadhaa na Lugha Kali toka
Clouds tv alonng side with my Boy Ttue oy